nmb

nmb

Thursday, March 27, 2014

Taswira toka Lake Manyara National park

Lake Manyara National Park - Tanzania
Eneo linalojulikana kama maji ya moto ambalo lipo pembezoni ya ziwa Manyara (linaloonekana kwa mbali). Asikwambie mtu, haya maji ni ya moto kweli kweli.. usiende kichwa kichwa kutest joto lake, unaweza ukaiona safari ya porini chungu.

Lake Manyara National Park - Tanzania
Mateja wakiwa wanapumzika mida ya mchana baada ya mihangaiko yao

Lake Manyara National Park - Tanzania
Japo ni kama mweusi lakini wanaitwa Blue Monkey akiwa Manyara NP.
Shukran ya picha kwa mdau Aenea

TIGO NGORONGORO MARATHON‏

Meneja Mawasiliano wa Tigo John Wanyancha akizungumza na waandishi wa habari mapema leo wakati wa kutangaza udhamini wa kampuni hiyo katika mbio za 'Tigo Ngorongoro Marathon' zitakazofanyika 19 Aprili 2014 wilayani Karatu, Ngorongoro - Arusha. Kushoto ni Mratibu wa mbio hizo, Datus Joseph, kutoka kampuni ya utalii ya Zara Tours.

Mratibu wa Matukio, Datus Joseph, kutoka kampuni ya utalii ya Zara Tours akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mbio hizo mapema leo.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tigo Ngorongoro Marathon kuchangisha fedha kwa ajili ya kukumbana na Malaria nchini
Dar es Salaam, 17 Machi  2014 – Mwaka wa saba wa ‘Tigo Ngorongoro Half Marathon’ iliyopewa kauli mbiu ya “Kimbia kuikabili Malaria” itafanyika Jumamosi ya 19 Aprili 2014 wilayani Karatu, jijini Arusha. Mbio hizo za kila mwaka inategemea kuwavutia wanariadha 3000 wa kitaifa na kimataifa, Tigo ilitangaza leo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Meneja Mawasiliano wa Tigo John Wanyancha, alisema kwamba Tigo Ngorongoro Marathon ni fursa ya kuhamasisha jamii kuhusu jinsi ugonjwa wa Malaria unavyoathiri watu milioni 300 mpaka 500 duniani, asilimia 90 wakiwemo barani Afrika.
“Malaria inaua zaidi watu milioni moja kila mwaka. Nchini Tanzania mtu mmoja anafariki kwa ugonjwa wa malaria kila baada ya dakika 10. Mbio za mwaka huu inahusisha pia harambee yakujenga kituo cha hospitali,” alisema Wanyancha.

Mwaka wa 7 wa mbio hizi za Tigo Ngorongoro Half Marathon inaambatana na maadhimisho ya Siku ya Malaria inayoadhimishwa tarehe 25 Aprili kila mwaka. Tukio hilo, kutokana na maelezo ya Wanyancha inategemewa kuzinduliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Lazaro Nyalandu kama mgeni rasmi.
Tigo inashirikiana na moja ya makampuni ya utalii yanayoongoza nchini kwa jina la Zara Tanzania Adventures, katika kuandaa mashindano haya, ambapo fedha  zitakazopatikana zitatumika kununua na kugawa neti za mbu, pamoja na kununua dawa za malaria ambapo zitagawiwa mahospitalini Arusha bure.
Fedha zitakazochangishwa pia mwaka huu zitatumika kukarabati vituo vya afya vilivyopo pamoja na kujenga kituo kipya cha afya kitakachoanzishwa Ngorongoro pamoja na shule ya awali katika vijiji tofauti tofauti kwa gharama ya shilingi milioni 160 jumla, alisema Wanyancha.

“Mbio za Tigo Ngorongoro half marathon sio tu  burudani kwa watu watakaoshuhudia bali ni sehemu nzuri sana yenye kuhamasisha kuhusu namna ya kujikinga na kutibu ugonjwa wa malaria kwa jamii inayozunguka maeneo ya Monduli na Arusha kwa ujumla,” alisema.

Mbio hizi zinawapa fursa wanariadha kukimbia katika sehemu moja yenye vivutio vya kipekee duniani, kutoka kivutio cha Ngorongoro mpaka jiji la Karatu. Mbio za mwaka huu pia inahusisha mashindano ya makampuni ya kilomita 5 kwa makampuni wenye nia yakuchangia katika harambee hiyo.
Kutokana na maelezo ya Mratibu wa Mbio hizo, Datus Joseph, kampuni zinazaodhamini mbio hizi katika ngazi za mashindano ya makampuni ni SBC Tanzania Ltd, CHUCHU, BG Tanzania, Hans Paul, Mberesero Lodge Tented Camps, Afrika-Safari, Orange gas na BIL

Tembo na Mwana Masikio ndani ya Serengeti




Manyara National Park

Ni Kundi la Makapela

Serengeti National Park
ukikutana na kundi la swala na wote wa pembe, jua hilo ni kundi la swala makapela. 

Serengeti National Park

Serengeti National Park

Mdau alishuhudia 'Live' hili windo la Wahadzabe


Hadzabe Hunters in Lake Eyasi Tanzania
Ni Mdau Thomas wa HSK Safaris ambaye alikuwa maeneo ya pembezoni mwa Ziwa Eyasi wanakoishi watu wa kabila ya Wahadzabe. Siku hii waliongozana na wenyeji (Wahadzabe) kwenda kwenye mawindo yao ya kujitafutia chochote. Kwa mujibu wa mdau Thom, huyu jamaa alimdungua huyu ndege (Hondohondo) kwa mshale mmoja tu. Shughuli nzima ilichukua kama dakika 10 hivi za kumnyatia na baada ya mshale kuchomoka, hondohondo alianguka chini mzima mzima.
Kwa tulio mjini na maeneo yaliyopiga hatua, mshale unaweza onekana kama zana duni lakini hawa Wahadzabe mshale ndio silaha yao kuu ya kuwindia na inaelezwa ya kwamba wana shabaha ajabu. Kabila hili wao hula nyama pamoja na matunda, majani au mizizi wanayookoteza porini. Hawalimi mazao kama jamii nyingine. Nyama wanayokula huipata kwa mawindo kama hili ambalo siku hii walimkaribisha Tom na wageni wake kulishuhudia. Ni Kabila mojawapo ambalo linawavutia wageni wengi kuwatembelea ili kushuhudia na kuona mfumo wao wa maisha kwa ukaribu. Wana mengi ambayo yatakuacha mdomo wazi na usiweze kuamini kuwa kwenye karne hii ya digitali kuna jamii zinaishi maisha kwa mfumo huu. Hawa ndugu zetu wanalinda na kudumisha mila zao kwa miaka na miaka. Hata ukienda kwenye mtandao Wikipedia (Bofya hapa) na kusoma habari za kabila hili utakutana na vitu vingi. Baadhi ndio kama hivi ambavyo mdau Thomas amekutana navyo hukoe Lake Eyasi wiki chache zilizopita.
Nyani na Ndegere wapo kwenye menu yao pia, na nimedokezwa na mdau kuwa endapo Nyani anakutana uso kwa uso na hawa jamaa wakiwa mawindoni, basi Nyani/Ndegere huanza kutoa milio ya ajabu hali ya kuashiria kupoteza matumaini. Wakikutana na Nyani hawamuachi na mshale ukitoka kwenye upinde basi subiri kusikia akidondoka chini muda mfupi baadae. Siku hii mdau Tom anasema kuwa kundi lao halikukutana na nyani wakati wa windo lao, badala yake jamaa wakawapa demo ya huyu Hondohondo kama anvyoonekana kwenye picha ya juu. Waliowatangulia siku moja kabla walipata bahati ya kushuhudia windo la Nyani na wanasema Nyani alitoa kilio cha ajabu sana baada tu ya kuwaona jamaa wakiwa karibu nae kwenye hali ya kumnyatia.

Hadzabe Hunters in Lake Eyasi Tanzania

Napenda kusisitiza tena, Utalii sio wanyama na mapori tu. Jamii nazo zina mengi ya kuweza kutufundisha na kutuelimisha na hata kukuburidisha. Kama utalii wa Mbuga na Maporini unauogopa basi hata huu wa mila na desturi sambamba na mambo ya kale na kihistoria unaweza kukupa mawili matatu yakakufanya uifahamu Tanzania vyema na ukaielezea vizuri zaidi kwa wasioifahamu. Picha ya pili ni Wanajamii wa Kabila la Wahadzabe wakipumzika na kupata kazi na dawa kabla ya kuendelea na shughuli zao za kutafuta chochote wakiwa sambamba na wageni wao. Picha zote na Mdau Thomas wa HSK Safaris
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

AddThis