nmb

nmb

Monday, March 25, 2013

Wanyamapori 15,000 wauawa nchini



Moshi. Zaidi ya wanyamapori 15,220 wameuawa na majangili katika hifadhi mbalimbali zilizopo chini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) katika kipindi cha miaka minne iliyopita wakiwamo tembo 419.

Kutokana na ukubwa wa tatizo hilo, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka alipendekeza kuundwa kwa kamati teule ya Bunge kuchunguza kuimarika kwa mtandao wa ujangili nchini.
“Ni mtandao wa kimafia ambao hata baadhi ya watendaji serikalini wanaujua, lakini wanauogopa sasa. Katika mazingira haya ni vyema Bunge likachunguza ni kina nani hawa ambao wanaogopwa,” alisema.

Kwa mujibu wa Mhifadhi Mkuu wa Tanapa, Mtango Mtahico, baadhi ya wanyama waliouawa kwa ajili ya kitoweo walikaushwa na kusafirishwa nje ya nchi zikiwamo nchi za Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Sudan.

Mtahico alisema katika wanyamapori hao 15,220 waliouawa na majangili kati ya mwaka 2009 na 2012, kwa ajili ya kitoweo wamo nyumbu, mbogo, nyamera, pofu, pundamilia, swala na wanyama wengine.

Mhifadhi huyo alitoa taarifa hiyo juzi katika kikao cha wadau wa uhifadhi Kanda ya Kaskazini kilichohudhuriwa na wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wabunge na wakurugenzi wa halmashauri.

“Ujangili huu wa wanyama ambao unaongezeka nchini unachochewa na mahitaji ya kitoweo na pia mahitaji ya kibiashara kama ya pembe za ndovu na faru duniani”alisema Mhifadhi Mkuu huyo.
Mtahico alisema katika miaka ya hivi karibuni, mitandao ya ujangili imekuwa ikijiimarisha na kutumia silaha za kivita, sumu na nyaya ambazo mpaka sasa hazijulikani zinatoka maeneo gani ya nchi.“Utafiti unaendelea kujua hizi nyaya zinatoka wapi maana zinakamatwa nyingi, lakini hazipungui na hizi hazichagui zikishategeshwa zinaweza kuua hata nyumbu 100 kwa mara moja,” alisema Mtahico.

Akizungumza katika mkutano huo wa siku mbili, mbunge wa Karatu, Israel Natse alilalamikia unyama unaofanywa na askari wa Tanapa wanaodhibidi ujangili akitaka wabadili mtazamo wa utendaji kazi.

“Rangers (askari) ni wanyama mno, vitendo wanavyofanya utadhani ni vitendo vile vilivyokuwa vikifanywa na Makaburu,” alisema Natse akilalamikia pia fidia ndogo kwa watu wanauawa na wanyama.

Kauli hiyo iliungwa mkono pia na mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari ambaye alisema kuna udhalilishaji mkubwa wanaofanyiwa wananchi wanaokutwa wakiwa ndani ya hifadhi hizo.

1 comment:

YASIN A . said...

You can do all dirty things, but you are just hurting yourself, as you have to know that, the end of all of this, the Parks will be empty, no Tourist and animals will run far away from you and what are you going to do?
Stop what you are doing and save our Countries jewels for the future generation.
And last, your parents did save those animals until you came to the World and why not you?
Do you think that you can replace those poor animals like plants? No way. Be good and do not accept to be SOLD to few who are intending to harm our Country and The GIFT we Received from our ancestors .

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

AddThis