nmb

nmb

Monday, September 17, 2012

HUYU NDIO KAKAKUONA WA AJABU ALIYEONEKANA HUKO WAARABUNI NA HUKO KILWA TANZANIA


mwananchi wa huko waarabuni akichukua picha ya kakakuaona kwenye simu yake


 
Mnyama Kakakuona akiwa amewekewa viu mbalimbali ili achague kimoja ambacho hutoa ishara ya kutokea kwa kitu hicho hapo mbeleni


Mnyama inayesemekana wa ajabu Kakakuona na ambaye huonekana kwa nadra sana ameonekana jana katika wilaya ya Kilwa mkoani Lindi. Mnyama huyo anapoonekana wanaomuelewa wanamuwekea vitu mbalimbali ikiwa kama kumtaka atabiri ni nini kitatokea kwa kipindi kijacho. kama akielekea kwenye maji wengi huwa wanadai ni mvua za kutosha. Jana katika vitu alivyowekewa mnyama huyo alielekea kwenye mtungi wa gesi na kuulambalamba ambapo kwa mujibu wa wachambuzi wa mambo hayo ya imani wanadai kutakuwa na gesi ya kutosha maeneo hayo na hasa ukizingatia tayari maeneo hayo yashagunduliwa gesi na inasubiriwa tu kazi ya uchimbaji iendelee.

Sina uhakika sana kama haya mambo ni kweli au ni mambo tu ya Imani mbofumbofu!1 kam ani kweli basi nadhani kila nyumba bongo itaatumia gesi na kusahau mkaa; magari yote bongo tutatumia gesi na kuachana na Kiwese ambacho kinapanda bei kila kukicha.

Kakakuona akiwa katika pozi

 
Kakakuona akiusogelea mtungi wa gesi

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

AddThis