nmb

nmb

Tuesday, April 23, 2013

SIMULIZI: ASIA DIGITALI SEHEMU YA 5


SIMULIZI: ASIA DIGITALI

MTUNZI: George Iron

SEHEMU YA TANO


Kijana hakukumbuka kama anayo pete ya ndoa, hakukumbuka kama anao watoto nyumbani.

Denny akachukua mkondo wa wanaume wengi, kuwa watumwa wa ngoni linapokuja suala la ana kwa ana na msichana.
Akamkumbatia Asia.
Ulikuwa mchezo wa dakika zisizopungua hamsini, sakafu ilihangaishwa, kitanda kiliteseka, bafu nalo liliona kilichotokea.
Deniss hakuwahi kufanyiwa manjonjo hayo na mkewe wa ndoa.
Walipotoka bafuni. Deniss akakumbuka kujibu swali.
“Nipo tayari kwa zawadi ya kwanza, nami nitakupa zawadi pia mpenzi.”
“Ok siku ukiipata hiyo pesa utanambia…” Asia akauliza swali la mitego.
“Sio kuipata ipo tayari..yaani siku ukiwa na nafasi tu my dear.” Deniss akajileta kwenye kumi na nane. Asia akachekelea maana hakuna mchezo alioupenda kama mchezo ndani ya kumi na nane.
“Basi tufanye kesho kutwa maana kesho nakimbia Mbeya…..narudi keshokutwa mchana…” alidanganya Asia ili aweze kujipanga kuchuma baada ya kupanda mwezi mzima.

****

DENISS aliondoka kurejea nyumbani akiwa na furaha ya aina yake. Hakuwa na moyo wowote wa majuto juu ya kitendo chake cha kufanya mapenzi na Asia wakati yu katika ndoa.
Alikuwa akiwaza kuwa ameweza kumzunguka mbunge fulani na kulala na mkewe. Nafasi ya kipekee kabisa.
Jambo jingine lililompagawisha ni uamuzi wa kushangaza wa Asia wa kumnunulia kiwanja na ikiwezekana kumsaidia katika ujenzi.
“Wabunge wetu wana pesa hawa pumbavu zao…” alitokwa na kauli hiyo Deniss huku akiwa makini na barabara.
Akiwa katika kumuwazia Asia mara ukaingia ujumbe katika simu yake, akasubiri alipoyafikia mataa ya kuzuia magari, akaichukua simu.
Alikuwa ni Asia ametuma ujumbe.
“I have never been fuc*ed like this. Thanx.”
Ujumbe ule mfupi, Deniss aliurudia mara mbilimbili, hakuamini hizo sifa alikuwa anapewa yeye.
Alikuwa amefanikiwa kumteka Asia kwa penzi la muda mfupi tu.
“Hapa huyu mbunge asahau kabisa kama ana mke. Na mimi ndo sitoki hapa.” Aliongea kwa sauti ya juu, tabasamu likiutawala vyema uso wake.

Deniss alitamani sana kuendelea kuwa na ujumbe ule katika simu yake, lakini tatizo alikuwa na mke. Akalazimika kuufuta huku moyo ukimuuma.


****


HATIMAYE baada ya mwezi mzima wa kujtengana na rafiki zake Asia alihitisha kikao cha dharula. Japo awali alitaka kuyamaliza mambo haya kimya kimya, lakini akajikuta harakati zake akimuhitaji mtoto wa kikurya Janeth, na wenzake wawili akiwemo Messi ambaye ni mtaalamu wa mipango.

“Jamani nimekuwa kimya mwezi mzima, najua mmechonga sana ooh Asia anaringa, sijui nini……hayaaishi midomoni nyie watoto kama Janeth ulivyokuwa mpana kama magagulo ya wasomali sikuezi.” Akazungumza Asia kwa nyodo, kimya kikatanda kisha kama wameambizana akaanza kucheka Janeth, Messi ambaye jina lake halisi ni Husna akafuatia, mara Asia, mwishowe meza nzima wakawa wanacheka.
“Imetosha sasa.” Aliwakatisha Asia.
“Nimeleta kazi mezani.” Alisita akagida maji kisha akaendelea, “Messi unamkumbuka jamaa uliyekutana naye benki mwezi ule.”
“Jamaa gani?” Husna akauliza.
“Yule ambaye ulinipa namba ya simu.”
“Eeeh nimemkumbuka vipi kwani?”
“Mambo yameiva ni sisi tu kupakua.” Asia aliwashirikisha wote kwa pamoja.
Akawasikiliza anasema nini.
Akausikiliza ushauri wa Husna, haukuwa ushauri mzuri sana, ushauri wa kumuibia Deniss kadi ya benki na kwenda kuvuta pesa.
“Hapana Messi hiyo mbaya…mi nataka ile ya kisasa mbona hiyo imekaa kinjaa njaa sana. Kama tunachuna mwanachuo banaaa.” Aligoma Asia.
Janeth alikuwa kama hawasikilizi vile, lakini aliponyan yua kinywa na kusema neno mambo yakaonekana kua sawa. Akakubaliana na Janeth.

Wakaagana huku wakiisubiri siku ya siku.

Milioni kumi.
Hazikuwa pesa ndogo. Isitoshe Asia hakuwa ametumia zaidi ya laki tano katika kufanikisha hili.

SIKU IKAWADIA.


ASIA alikuwa ameikalia vyema gari aina ya Harrier, alikuwa anaikanyaga vyema kana kwamba ni ya kwake.

Ndani ya gari aikuwa yeye na Deniss, siku hiyo Asia aligoma kutumia gari ya Deniss alihitaji naye kumuendesha.
“Mapenzi ya kihindi haya…” alijisemea Deniss wakati akikubaliana na Asia.
“Au umechukia baby.” Asia alibembeleza kiwiziwizi.
“Hamna jamani mbona sawa tu…” alijibu Deniss.
Sasa alikuwa katika gari la Asia, ilikuwa ni saa sita mchana.
“Tuanzie kwangu ama kwako.” Asia aliuliza ka kuridhika akia anaikanyaga gari kwa umakini.
“Mh. Kwani we unachukua wapi?”
“Standard chattered Posta kule.” Alijibu Asia.
“Mimi Crdb yoyote tu…lakini huwa napendelea ya kule mtaa wa Lumumba. Hakuna foleni na uhakika wa pesa ndefu upo.”
“Pesa ndefu? Kwako pesa ndefu ni ipi? Hao CRDB walioshindwa kunipa ki milioni hamsini kwa wakati unasema wanatoa pesa ndefu? Benki za kibongo ushenzi tu…walinifanya nionekane mwongo mbele za watu ” alijibu Asia ka kuonyesha kukereka.
Deniss, kimya aliogopa kujibu kitu maana kwake pesa ndefu alihesabia hiyo milioni kumi, kumbe mwenzake aliwahi kukosa ki-milioni hamsini.
Ipi pesa ndefu sasa?.
Deniss hakujua kama mfumo wa digitali hauhitaji kupandisha antenna juu ili kuondoa chenga chenga. Hakujua kama ni kuseti kidogo tu king’amuzi na mambo yanaenda sawa.
Deniss naye alikuwa analojia.

Wakalifikia ghorofa kubwa ambalo chini kuna benki ya Standard chattered…….

“Tushuke basi si unajua kuna kukabwa……’ Asia akamsihi Deniss. Wakashuka.
Ðeniss aliposhuka, asia akamfuata na kumnong’oneza kwa tahadhari.
“Jiweke mbali kidogo si unajua tena wavimba macho, nisije nikatolewa magazetini nikaivunja ndoa.” Maneno yale yakamtia wivu mkali Deniss, Asia alihitaji sana hali ile.
Akazama ndani ya benki Asia, akamwacha Deniss amekaa mbali kabisa akiwa hana habari na yule binti.
Asia akajaza karatasi kadha wa kadha.
Deniss akiwa amezubaa katika gazeti mara ukaingia ujumbe.
“Njoo unisaidie.’ Mtumaji alikuwa Asia. Deniss akaangaza huku na kule akamwona, akasimama na kumfuata.
“Nisaidie kujaza” Asia alisema kwa sauti ya kimahaba.
Deniss akaanza kujaza.
“Nitolee 45 kabisa. Nimekumbuka nina safari juma lijalo.” Asia alimpa maelekezo Dennis, Deniss akajaza milioni arobaini na tano kutoa.
Asia akachukua ile karatasi akaenda dirishani.
Akafanya tukio la sekunde kadhaa.
Akabadili karatasi.
Akamkabidhi yule dada aliyekuwa dirishani.
Akamkabidhi na pesa kiasi cha shilingi elfu hamsini.
Alikuwa anaweka katika akaunti ya Janeth.
Aliporudishiwa ‘paying slip’ akafungua koba lake kwa mbwembwe akaweka ndani.
Akatoa karatasi nyingine tena akamkabidhi yule muhudumu.
Akaweka elfu thelathini katika akaunti ya Husna.
Nayo kama ile ya awali akatia karatasi katika koba lake.
Mchezo ulienda kama alivyotaka.
Akasogea pembeni akazugazuga kisha akaondoka.
“Twende zetu afisa.” Alimshtua Deniss.
Wakatokomea.

Walipoifikia zamu ya Deniss kutoa pesa ikazuka ile dhana ya wanaume wengi kupenda sifa mbele ya msichana hasahasa akiwa mrembo. Sifa hizi za kijinga huwatokea wanaume wengi puani, yaani hupenda kujionyesha kuwa wana pesa nyingi, kujidai kuwa hawajali hata pesa zao zikitumika hovyo.

Lakini mwisho wa siku akilala kitandani anasema. NINGEJUA.
Pepo hilo likamkaba Deniss pia.
Akataka kujiweka daraja moja na Asia.
“Na mimi njoo unisaidie.” Alijifanya kudeka.
Asia ambaye katika filamu hii ni mke wa mbunge, akarembua jicho. Kisha akachukua kalamu.
Alipofikia kiwango cha kutoa.
“Nitolee kumi na tano kuna jambo nataka kufanya na hiyo tano.”
Asia akacheka kidogo kisha akamjazia, moyoni akafurahia dau kupanda.
Deniss akapanga foleni, baada ya nusu saa akarejea akia na bahasha yenye chapa ‘CRDB BANK’
Ujazo wake ulikuwa wa kulidhisha.
Asia akarukwa na mate mdomoni, lakini kama alivyoanza taratibu alitaka kumaliza hivyohivyo.
Wakaondoka.
“Yaani pesa bwana hicho hapo kimilioni kumi na tano eti….duuh.” alisema Asia huku akiingalia ile bahasha kwa dharau kiasi.
Deniss hakujibu.

Akiwa anaendesha mara simu ikaita.

Akaegesha gari pembeni kidogo. Akapokea.
Ilikuwa simu ya kuigiza kutoka kwa mmiliki wa kiwanja ambacho walikuwa wanaenda kununua.
“Wakati mwingine nachukia kufanya biashara na wabongo.”
“Kuna nini?”
“Eti hadi saa kumi na mbili, sijui kuna mambo gani gani aaargh. Fuck” alighafirika.
Deniss akaanza kushusha chini kihulka. Alifanya vile kama anafanya kwa mpenzi wake wa siku nyingi.
“Baby…nahitaji kupumzika pliiz…..we have to go somewhere..we unadhani sasa hivi saa nane hadi ifike saa kumi na mbili ni leo…”
Kauli hiyo ikamfurahisha Denny, akaikumbuka ile siku alipoonja tunda la mke wa mbunge.
Kama alivyotaka Asia baada ya saa zima walikuwa ndani ya chumba wakila raha.
Deniss kichwani akiamini kuwa ndani ya kile chumba kuna milioni hamsiniAsia ndiye aliyeijua hesabu sahihi.
Asia Digitali akachezesha kiuno kwa umakini huku akicheza na muda, alimpa Deniss kitu roho inapenda akamzidishia makusudi viuno ili afikie lengo.
Lengo la kumchosha.
Kweli akachoka mwishowe akalala.
Asia naye akazuga kulala.
Akamshtua Denis saa kumi na mbili na nusu.
Walikuwa wamechelewa.
Wakajiandaa upesi wakatoweka.
Asia akiwa ameukamata usukani.
Wakapita hapa na pale.
Foleni ikawa kikwazo Asia akaamua kupitia njia za panya, ni huku walipokutana na dhahama.
Wakakutana na gari nyingine, hakuna aliyetaka kumpisha mwenzake.
Kigiza kile kila mmoja akammulika mwenzake.
Asia akaghafilika. Deniss akagundua hilo.
Ama kwa hakika ukitaka mwanaume apigane basi mdharau mbele ya msichana.
Deniss akashuka mbiombio kuwakabili wale walioziba njia.
Asia naye akashuka.
Akakutana na kimya cha hatari.
Mara akazolewa mtama. Akatua chini kama mzigo alipojaribu kupiga kelele alikutana na mdomo wa bunduki.
Kidogo Asia acheke kwa jinsi Deniss alivyokuwa anatetemeka lakini akaumbuka kuwa alikuwa katika kuigiza filamu.
Hakutakiwa kucheka, akaendelea kulia.
Mmoja kati ya watekaji akaiendea gari. Badala ya kupekua akaiwasha. Ikaunguruma kisha ikageuzwa na kupotea.
Deniss alikuwa amejikojolea tayari.
Watekaji walificha nyuso zao.
Wawili walikuwa wanaume. Mmoja mwanamke.
“Ole wako usimame.” Alipewa onyo Deniss aliyekuwa amelala chini.
Asia kitambo alikuwa amejifanya kuzimia. Alikuwa ametulia tuli.
Baada ya dakika kumi eneo lile lisilokuwa na nji za magari walikuwepo watu wawili, Asia na Deniss.
Deniss alikuwa amepagawa.
Lazima apagae, hakutegemea shambulizi hili, halafu mbaya zaidi wameondoka na gari la Asia na pesa zote......kizungumkuti
Alijaribu kumwamsha Asia, hakuamka. Akamtikisa lakini hali ikawa vile vile.
Deniss akaamua kujijali kwanza yeye, Asia baadaye, akatimua mbio kali.
Kuna kichwa kilikuwa kimejibanza mahali kikisubiri jambo hilo litokee.
“Amka wewe bwege kasepa.” Sauti tulivu ya Janeth maji ya shingo.
Asia akainuka, akasahau viatu, pekupeku akajikongoja.
Wakaikuta taksi inawasubiri.
Wakatokomea.
“Janeth wewe mbayaaaa.” Asia alimsifu mkurya yule.

***KI-DIGITALI ….mtu anasuka mwezi mzima…lakini malipo yake sasa…….usiombe kukutana naye…….utajuta kuzaliwa…..


ITAENDELEA……itaishia hapa kwenye hii blog unaweza kununua hiki kitabu namna ya kununua cheki upande wa kulia wa blog yako kuwasiliana na mtunzi

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

AddThis