nmb

nmb

Monday, May 6, 2013

FAHAMU ZAIDI KUHUSU KUFUTWA KWA MATOKEO YAKIDATO CHA 4


wanafunzi
Serikali ya Tanzania, imeagiza mitihani yote ya kidato cha nne kwa mwaka 2012, kusahihishwa upya baada ya Tume iliyoundwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda ya kuchunguza sababu zilizosababisha matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 kuwa mabaya, kuwahi kutokea katika historia ya mitihani Tanzania.

Asilimia 60 ya watahiniwa walianguka mitihani hiyo na kusababisha serikali kuunda tume ya uchunguzi baada ya wadau wa elimu, wazazi na wanafunzi kulalamikia matokeo hayo.
Tume hiyo ilichunguza sababu zilizosabisha matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 kuwa mabaya, na imependekeza kwa serikali kufuta matokeo yote ya mitihani hiyo na isahihishwe upya.
Uamuzi huo umetangazwa katika kikao cha Bunge la Tanzania linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaye shughulikia Sera na Uratibu, William Lukuvi.
Tume hiyo, ilipewa hadidu za rejea kadhaa ikiwemo kutafuta sababu za matokeo mabaya ya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012; Kubaini sababu za kushuka kwa kiwango cha ufaulu katika mitihani ya Kidato cha Nne mwaka 2011 hadi 2012; Kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua kukabiliana na tatizo la mwenendo wa kushuka kwa kiwango cha elimu mara moja,kipindi cha muda mfupi, kati na kipindi cha muda mrefu.

Pia Tume hiyo ilipewa jukumu la kutathmini nafasi ya Halmashauri katika kusimamia Elimu ya Sekondari katika Halmashauri zake; na kuanisha sababu nyingine zinazoweza kuwa zimechangia hali hii ya matokeo.
Tume imebaini pia kwamba, pamoja na Wanafunzi hawa kuwa katika mazingira yanayofanana na ya wenzao wa miaka iliyopita na kwamba ufanisi katika shule kwa ujumla umekuwa unashuka kwa sababu mbalimbali,zikiwemo za mabadiliko ya mchakato wa kuandaa na kutoa matokeo ya mtihani kwa mwaka 2012. 

Mfumo uliotumika mwaka 2012 katika kupanga matokeo na madaraja ni tofauti na ule uliotumika mwaka 2011 na miaka iliyotangulia.

Hata hivyo baadhi ya wadau wa elimu, wazazi na wanafunzi wamehoji uamuzi huo wa serikali kama hautakuwa na athari kwa wanafunzi waliofaulu na kujiandaa na masomo ya kidato cha tano na wale ambao tayari wamejiandikisha kurudia mitihani yao kwa njia ya kulipia

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

AddThis